1. Tangazo linaonyesha nini? Andika maelezo ya watu wa picha.
2. “Unyanyapaa” ni nomino inayotokana na kitenzi “kunyanyapaa.” Maanake ni nini?
3. Chini ya picha, unaona mifano miwili ya sarufi ya dhamira tegemezi: “tusimtenge” na “aendelee.” Kwa nini dhamira tegemezi inatumiwa katika mifano hii?
4. Kwa nini jina la tangazo hili ni “Unyanyapaa na UKIMWI”? Kuna uhusiano gani baina ya mambo haya mawili?
5. Ukiunganisha picha na maneno ya tangazo hili, unafikiri lengo lake ni nini?